Imani ya Kuomba Mpaka Kupokea na Mwl. Eng. Peniel Sarakikya

TZS 10,000.00
In stock
SKU
SpImani ya Kuomba Mpaka Kupokea na Mwl. Eng. Peniel Sarakikya

Maudhui ya kitabu hiki ni kufufua ari yako ya kuomba, na 
kukupa mwongozo wa kuomba kwa usahihi. Somo 
hililimefunua siri ya kuishi kwa utoshelevu kwa njia ya 
maombi. Utajifunza Maelekezo ya Yesu Kristo kuhusu 
Maombi. Utazijua Sifa za Imani ya Kuomba hadi kupokea. 
Utaelewa Kanuni za Kuomba kwa usahihi.  
Utajua Vikwazo vya maombi yako na namna ya 
kukabiliana navyo. Kupitia somo hili utajifunza Umuhimu 
wa Kumpa Roho Mtakatifu nafasi katika maombi yako. 
Utatambua majira na wakati ufaao kumwomba Mungu na 
Umuhimu wa kujiwekea akiba ya maombi.  

Imani ya Kuomba Mpaka Kupokea na Mwl. Eng. Peniel Sarakikya

Kuna wakati ubongo hubishana na moyo juu ya uhalisia 
wa tatizo fulani. Moyo hukaa na hisia na ubongo hukaa 
kwenye ukweli.  
Mabishano ya pande hizi mbili yakiwa makali, Mungu 
huingilia kati kushawishi taratibu, lakini shetani 
hulazimisha kwa nguvu matakwa yake.  
Ubongo hufika mahali na kusema "litakalo kuwa na liwe", 
moyo nao husema "tatizo bado halijaisha".  
Katika mazingira haya, wale wanaokumbuka kuutafuta 
uso wa Mungu kwa maombi huibuka washindi, na wale 
wanaoishia kuwaza sana bila kuomba hukata tamaa 
Hakuna mwanadamu aliyetosheka. Kila mmoja wetu ana 
kitu cha ziada anachotafuta. Watu wengi hutumia juhudi 
za kimwili kutafuta wanayohitaji, lakini wengi hukosa 
kutokana na sababu nitakazokueleza katika kitabu hiki.  
Wapo ambao hukosa kwa sababu hawamwombi Mungu 
kabisa. Wapo ambao hukosa kwa sababu huomba 
vibaya.  

Maudhui ya kitabu hiki ni kufufua ari yako ya kuomba, na 
kukupa mwongozo wa kuomba kwa usahihi. Somo 
hililimefunua siri ya kuishi kwa utoshelevu kwa njia ya 
maombi. Utajifunza Maelekezo ya Yesu Kristo kuhusu 
Maombi. Utazijua Sifa za Imani ya Kuomba hadi kupokea. 
Utaelewa Kanuni za Kuomba kwa usahihi.  
Utajua Vikwazo vya maombi yako na namna ya 
kukabiliana navyo. Kupitia somo hili utajifunza Umuhimu 
wa Kumpa Roho Mtakatifu nafasi katika maombi yako. 
Utatambua majira na wakati ufaao kumwomba Mungu na 
Umuhimu wa kujiwekea akiba ya maombi.  
Ni maombi yangu, kwamba Roho Mtakatifu 
atakuwezesha kuelewa na kuutendea kazi ujumbe huu.  
Mwl. Eng. Peniel S. Sarakikya  
April 2024
 

More Information
Seller SARAKIKYABOOKSTORE
Author Mwl. Eng. Peniel Sarakikya
Total Pages 141
Publisher Kiwonyi Printers
Write Your Own Review
You're reviewing:Imani ya Kuomba Mpaka Kupokea na Mwl. Eng. Peniel Sarakikya
Your Rating
We found other products you might like!
Copyright © 2023 - 2024 Mahali Sokoni Trading Company Limited. All rights reserved.