Urafiki na Uchumba

TZS 10,000.00
In stock
SKU
SpUrafiki na Uchumba

Safari ya ndoa huanza na uhusiano. Uhusiano 
unaanza kwa kufahamiana.  Kufahamiana 
kunaanza na urafiki.  Mtu anaweza kukupenda, 
lakini si muhimu awe rafiki, kwani marafiki 
huchaguliwa. Watu wengi wanaingia katika 
uhusiano wakiwa na matazamio mengi pasipo 
maandalizi ya kutosha. 

Urafiki Na Uchumba

Safari ya ndoa huanza na uhusiano. Uhusiano unaanza kwa kufahamiana.  Kufahamiana kunaanza na urafiki.  Mtu anaweza kukupenda, 
lakini si muhimu awe rafiki, kwani marafiki huchaguliwa. Watu wengi wanaingia katika uhusiano wakiwa na matazamio mengi pasipo 
maandalizi ya kutosha. Kuna matatizo mengi yanayotokea katika ndoa nyingi siku hizi. Uzoefu unaonesha kuwa, matatizo mengi yanayopelekea 
kuvunjika kwa ndoa nyingi yanatokana na sababu kuu tatu zifuatazo;


 • Kukosekana kwa maamuzi makini wakati wa kutaka kuoa au kuolewa.
 • Malezi na makuzi mabaya wakati wa utoto.
 • Kukosekana kwa ufahamu na maarifa ya kutosha kuhusu taasisi ya ndoa.
 

Maisha ni hatua. Maisha yenye mafanikio yanahitaji utaratibu, subira na uvumilivu. Vijana wengi siku hizi huanza uhusiano wa kimapenzi 
mapema kabla ya ndoa. Hivyo, inapofika hatua ya kufunga ndoa huwa hakuna jipya.Wengi wao 
wanakuwa wamezoeana, bahati mbaya sana hata kutubu kwa mwenyezi Mungu wanasahau. Hali ilivyo sasa, vijana wengi wameoa au kuolewa 
na watu wasio halisi na sahihi. Wako waliohusiana na watu ambao wamekuwa vikwazo katika maisha yao. Wengi wamehusiana na watu ambao 
wamefisha ndoto zao, malengo na maono yao; wameua imani katika Mungu na kuondoa furaha yao.  

Kukurupuka, matazamio yasiyo halisia, ulevi wa mapenzi na kukosa umakini vimewagharimu vijana wengi. Vijana wengi hawafahamu tofauti 
iliyopo kati ya kipindi cha urafiki na kipindi cha uchumba. Tunashuhudia siku hizi vijana wengi wakiwa wachumba na kuamua kuoana 
hata bila kupitia hatua ya urafiki. Ni muhimu ifahamikie kuwa, kipindi cha urafiki ni kipindi cha kumfahamu mtu vizuri zaidi kuliko kipindi cha 
uchumba, kwani wakati wa uchumba watu wengi huficha uhalisia wao. Majira ya urafiki na uchumba ni tofauti. Kijitabu hichi cha urafiki na uchumba kitawasaidia vijana kujitambua na kutofautisha majira ya urafiki na uchumba ili kufanya maamuzi sahihi kwa wakati 
sahihi na kwa mtu sahihi.

More Information
Seller MLYUKA BOOK STORE
Author Rev.Dr. Enock E Mlyuka
Total Pages 33
Publisher Rev.Dr.Enock E Mlyuka
Write Your Own Review
You're reviewing:Urafiki na Uchumba
Your Rating
Copyright © 2023 - 2024 Mahali Sokoni Trading Company Limited. All rights reserved.